FM Manyara

DC Lulandala awataka vijana kuchangamkia fursa ya mikopo inayotolewa na serikali

8 August 2025, 12:26 pm

Picha ya Mkuu wa wilaya ya Simanjiro mkoani Manyara Faki Lulandala

Mkuu wa wilaya ya Simanjiro mkoani Manyara Faki Lulandala, amewataka wakulima, wavuvi na wafugaji kutumia fursa ya mikopo inayotolewa na halmashauri kukuza mitaji Yao na kujiinua kiuchumi.

Na Mzidalfa Zaid

Lulandala ametoa wito huo mkoani Arusha ,alipokuwa mgeni rasmi wa zamu katika maonesho ya wakulima kanda ya kaskazini yanayoendelea  katika viwanja vya Themi Njiro, amesema  serikali ya awamu ya sita imetoa fursa ya kutoa mikopo ya asilimia 10 kwenye halmashauri zote nchini,hivyo vijana  wanaotaka mikopo hiyo wajiunge kwenye vikundi na wanufaike na mikopo hiyo, huku akisema amefurahishwa na ubunifu ambao umefanywa na washiriki wa maonesho hayo.

sauti ya Mkuu wa wilaya ya Simanjiro mkoani Manyara Faki Lulandala

Kwa upande wake mkurugenzi wa halmashauri ya mji wa Babati Shaaban Mpendu, amesema halmashauri yake imeshiriki maonesho hayo kwa  kutoe elimu kwa wakulima na wafugaji namna ya kulima na kufuga kisasa.

picha ya halmashauri ya mji wa Babati Shaaban Mpendu
sauti ya mkurugenzi wa halmashauri ya mji wa Babati Shaaban Mpendu

Baadhi ya washiriki wa maonesho hayo, wamesema maonesho ya mwaka huu yamekuwa makubwa kwa kuwa wananchi wengi wanatembelea mabanda  kujionea bidhaa zinazopatikana katika maonesho hayo huku wakielezea namna wanavyoyatumia maonesho hayo kutangaza biashara zao.

sauti ya washiriki