FM Manyara
FM Manyara
17 April 2026, 12:25 am

Na George Augustino.
Mkuu wa wilaya ya Babati Mkoani Manyara EmanuelaKkaganda amewaomba viongozi wa dini kuendelea kuzuia mmomonyoko wa maadili katika jamii kwa mafundisho ya imani pamoja na kuiombea amani nchi ya tanzania ili amani na utulivu uzidi kutawala.
Dc Kaganda ameyasema hayo leo katika sherehe ya uzinduzi wa Parokia mpya Mtakatifu Anna ya Mrara ya Jimbo Katoliki la Mbulu, sherehe iliyohudhuriwa na Askofu mwenyeji wa Jimbo Katoliki la Mbulu Mhashamu Baba Askofu Anton Lagwen, Askofu wa jimbo katoliki la Geita Flavian Kasala, Askofu wa Jimbo Katoliki la Bunda Simon Masundora, Mapadre mbalimbali pamoja na waumini wa Parokia mbalimbali ikiwemo Parokia mpya ya Mrara.
Kwa upande wake Muasham Baba Askofu wa Jimbo Katoliki la Mbulu Anton Lagwen amezindua na kuitangaza rasmi parokia ya mrara kuwa parokia kamili pamoja na kumtangaza Padre Yuda Aley kuwa Paroko wa kwanza wa Parokia hiyo mpya ya Mrara.

Mwaka 2023 Muasham Baba Askofu Anton Lagwen alikipandisha hadhi kigango cha Mrara na kuwa Parokia ndogo na mwaka 2024 akaipandisha hadhi Parokia ndogo ya Mrara na kuwa Parokia teule ya mrara yenye Jumuiya ndogo ndogo 10 na jumla ya waumini 1,261 kwa mujibu wa Sensa ya mwaka 2025 na hatimaye leo kutangazwa kuwa parokia kamili ya Mrara.
