FM Manyara
FM Manyara
6 June 2025, 5:34 pm

Wakulima mkoani Manyara wametakiwa Kutumia mbegu za asili kwenye kilimo ili kupata faida na kunufaika na mazao yake.
Na Marino Kawishe
Shirika lisilo la kiserikali la Pelum Tanzania limewataka wakulima wilayani Babati mkoani Manyara kuendeleza kilimo cha mbegu za asili ambacho kimekuwa na tija kwa baadhi ya maeneo hapa nchini.
Akizungumza na wakulima wadogo wa vijiji vya Endagile, Mwinkantsi, Kwaraa na Mamire katika maonesho ya mbegu za asili, afisa miradi na masuala ya jinsia kutoka shirika hilo Anna Marwa amesema lengo lao nikuona wakulima hao wakinufaika zaidi na kilimo cha asili.
Kwa upande wake afisa miradi kutoka COSITA mkoani Manyara Agustino Baloh amewaasa wakulima kutumia elimu ya kilimo asili kwa kushirikisha wanafunzi wanaosoma kwenye shule za msingi ili wapate uelewa wa kilimo hicho.
Aidha wakulima wa kilimo cha mbegu za asili wamelishukuru shirika la PELUM TANZANIA na COSITA kwa elimu waliyotoa kwenye maeneo yao ambayo imewawezesha kuendeleza kilimo cha asili ambacho kimekuwa na faida kwao.
