FM Manyara

Sekretarieti ya maadili ya viongozi wa umma yaendesha mafunzo  kwa waalimu na walezi wa club za maadili Manyara

21 April 2026, 6:40 pm

picha ya baadhi ya walimu

Taasisi ya sekretarieti ya maadili ya viongozi wa umma imeendesha mafunzo kwa waalimu walezi wa club za maadili, yenye lengo la kuzifahamu sheria ya maadili, katika sekta ya umma pamoja na muongozo wakufungua klabu za maadili katika shule za msingi hadi vyuo vikuu vilivyopo mkoani Manyara. 

Na Marino Kawishe

Akifungua mafunzo hayo ya siku moja katibu tawala mkoa wa Manyara Mariam Muhaj  ameitaka  kada ya waalimu kuendelea  kwa moyo mmoja kufundisha  maadili kwa wanafunzi kwakua wazazi wamekuwa  wakijishughulisha na shughuli za utafutaji  kutafuta  fedha na kujisahau kwenye malezi.

sauti ya katibu tawala mkoa wa Manyara Mariam Muhaj 
picha ya katibu tawala mkoa wa Manyara Mariam Muhaj 

Aidha kwa upande wake katibu msaidiz sekretarieti ya maadili ya umma kanda ya kaskazini Gerald Mwaitebele amesema lengo la mafunzo hayo kwa waalimu hao ni kuwajengea zaidi uwezo waalimu ambao ndio  wanafundisha watoto kutoka ngazi ya chini ili baadae vijana hao wanapoingia katika mitaa wawe na maadili mema.

sauti ya atibu msaidiz sekretarieti ya maadili ya umma kanda ya kaskazini Gerald Mwaitebele

Nae Kaimu Afisa Elimu Mkoa wa Manyara Mugisha Garibona amekiri kupokea maelekezo ya Katibu tawala mkoa wa Manyara aliyeagiza mkoa mzima kuwepo na Klabu za wanafunzi zinazofundisha Maadili ya Viongozi wa umma.

sauti ya Kaimu Afisa Elimu Mkoa wa Manyara Mugisha Garibona

Semina hiyo imewaleta pamoja waalimu wa shule mbali mbali za msingi na sekondari ambazo tayari zimeanzisha vilabu katika shule zao zinazofundisha maadili ya Viongozi wa umma kutoka Halmashauri tano za mkoa wa Manyara. 

picha ya viongozi sekretarieti ya maadili ya viongozi wa umma, katibu tawala mkoa wa Manyara na baadhi ya walimu