FM Manyara
FM Manyara
12 July 2026, 1:16 pm

Vijana katika Halmashauri ya wilaya ya Babati mkoani Manyara wametakiwa kutokujihusisha na makundi mtandao ambayo hutumika kuchochoea vurugu na kurudisha maendeleo nyuma.
Na Marino Kawishe
Akifunga mafunzo ya siku nne ya jukwaa la Vijana katika halmashauri ya wilaya ya Babati kaimu mkuu wa Wilaya ya Babati Remidius Mwema Emanuel amesema kuwa jukwaa hilo limewakutanisha vijana pamoja ili kuona ni kwa namna gani changamoto mbali mbali zinazowakabili zinatafutiwa ufumbuzi na kuona maendeleo yao yanakuwa.
Nae mkuu wa Idara ya maendeleo kutoka Halmashauri ya wilaya ya Babati January Bikubwa akawaasa vijana kuwa wajifunze kila siku na kufanya kazi kwa nidhamu huku akiwataka kutokulalamikia mazingira.
