FM Manyara

Wanaushirika Manyara watakiwa  kuzingatia uadilifu

14 May 2026, 4:59 pm

Picha ya baadhi ya viongozi wa vyama vya Ushirika

Wanaushirika mkoani Manyara wametakiwa kuendesha shughuli  za ushirika kwa kuzingatia uadilifu na kutimiza majukumu yao kama sheria zinavyoelekeza katika usimamizi  wa vyama vya ushirika.

Na Mzidalfa Zaid

Wito huo umetolewa leo na mrajisi msadizi wa vyama vya ushirika mkoa wa Manyara Absalom Cheliga wakati akiongea katika  jukwaa la maendeleo ya vyama vya ushirika mkoa wa Manyara.

sauti ya mrajisi msadizi wa vyama vya ushirika mkoa wa Manyara Absalom Cheliga
picha ya mrajisi msadizi wa vyama vya ushirika mkoa wa Manyara Absalom Cheliga

Kwa upande wake mwenyekiti wa jukwaa la ushirika mkoa wa Manyara Ramadhani Ismail amesema tangu kuanza kwa jukwaa hilo  mkoa wa Manyara umenufaika kutokana na elimu ambayo imekuwa ikitolewa kwa wanaushirika kama inavyoelekezwa katika misingi ya ushirika.

sauti ya mwenyekiti wa jukwaa la ushirika mkoa wa Manyara Ramadhani Ismail
picha ya mwenyekiti wa jukwaa la ushirika mkoa wa Manyara Ramadhani Ismail

Nao baadhi ya wanaushirika ambao wameudhuria katika jukwaa hilo, wamesema wamenufaika na elimu ambayo imetolewa jinsi ya kuendesha vyama vya misingi pamoja na kuwaelimisha wanachama umuhimu wa vyama vya ushrika.

sauti ya baadhi ya washiriki
picha ya baadhi ya washiriki