FM Manyara

Yas, Mixx by Yas Tanzania wazindua mnara wa mawasiliano  wa 4G na 5G Kiteto

20 July 2026, 5:03 pm

Picha ya mnara pamoja na baadhi ya wananchi

Zaidi ya wananchi elfu 8 katika kijiji cha ngeju kilichopo kata ya Namelock wilayani Kiteto mkoani Manyara kunufaika na mnara wa mawasiliano wenye uwezo wa 4G na 5G

Na Marino Kawishe

Kampuni ya simu za mikononi ya Yas  na Mixx By Yas Tanzania wamezindua mnara wa mawasiliano wenye uwezo wa 4G na 5G ambao utawanufaisha zaidi ya wananchi elfu 8 katika kijiji cha ngeju kilichopo kata ya Namelock wilayani kiteto mkoani Manyara. 

Akizungumza kwenye hafla ya uzinduzi wa mnara huo mkuu wa kanda ya kaskazini kutoka mtandao huo Robert Sanyagiamesema lengo la kampuni hiyo nikutoa huduma za mawasiliano zitakazowanufaisha wananchi kiuchumi ikiwemo kutoa na kuweka pesa, na kuwasiliana kikamilifu bila kikakwazo cha mtandao. 

Sauti ya mkuu wa kanda ya kaskazini kutoka mtandao huo Robert Sanyagi
Picha ya mkuu wa kanda ya kaskazini kutoka mtandao huo Robert Sanyagi

Kwa upande wao wananchi wa kijiji hicho wamekiri mtandao wa Yas  Tanzania utawanufaisha na kutatua kero za mawasiliano ambazo zilikuepo hapo awali kwenye eneo hilo.

Sauti ya wananchi

Nae Mwenyekiti  wa kijiji cha ngeju, Petro Singero amewashukuru viongozi wa kampuni  hiyo ya simu  za mkononi kwakuona fursa na kuwekeza  mnara huo kwenye kijiji  hicho ili kuwaondolea  changamoto  iliyokuwepo kwa muda mrefu ya kimtandao.

Sauti ya Mwenyekiti  wa kijiji cha ngeju, Petro Singero

Aidha,kuzinduliwa kwa mnara huo wa mawasiliano ya simu za mkononi wa kampuni ya Yas Tanzania kuna fanya mkoa wa Manyara kuwa na zaidi ya minara 100 inayohudumiwa   na Yas kwa kutoa huduma kwa wananchi na  ambayo imewekeza  zaidi ya shilingi Trillion moja hapa  nchini na kuwa ni kampuni  yenye  zaidi ya minara elfu 4800 yenye kasi ya 4G  plus mpaka sasa.

picha ya baadhi ya wananchi