FM Manyara
FM Manyara
3 July 2026, 7:15 pm

Na Marino Kawishe
Shirika la So They Can Tanzania limekabidhi miradi miwili ambayo ni bweni la wasichana na nyumba Tatu za waalimu zenye thaman ya zaidi ya shilingi milion 265, kwa halmashauri ya wilaya ya Babati mkoani Manyara ambayo imekamilika kwa asilimia mia moja.
Akizungumzia miradi hiyo mbele ya mgeni Rasmi Naibu Spika Daniel Sillo, Meneja mkazi wa shirika hilo Roselyne Mariki amesema kukamilika kwake ni utekelezaji wa mpango wa shirika hilo kwenye kuboresha miundo mbinu ya sekta ya elimu ambayo inatekelezwa katika kata nne za halmashauri ya wilaya ya Babati na ambayo inaungwa mkono na wananchi wa maeneo hayo.

Kwa upande wa Mgeni Rasmi Kwenye Halfa hiyo Naibu Spika Wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Daniel Baran Sillo amemshukuru Rais Samia Suluhu Hasan kwa kuendelea kuboresha mazingira ya Uwekezaji na kuvutia mashirika binafsi kufanya shughuli zao hapa Nchini.
Kwa upande wao wanafunzi pamoja na mwalimu wa shule ya msingi Manyara inayopakana na hifadhi ya Tarangire wametoa pongezi zao kwa shirika la So They Can Tanzania kwa kuwawezesha kupata nyumba za waalimu.
Aidha kukamilika kwa mradi huo kutawawezesha wanafunzi wanaokaa mbali hasa wa kike kufanya vizuri katik masomo yao na kuondokana na changamoto za vishawishi vinavyopelekea kupata ujauzito na kusitisha masomo yao.
