FM Manyara

EWURA yawahimiza wananchi kuwekeza vituo vya mafuta vijijini

29 July 2026, 6:44 pm

Picha ya Menejea wa EWURA kanda ya kaskazini George Mhina

Meneja wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) Kanda ya Kaskazini, George Mhina, amewahimiza wananchi na wawekezaji kutumia fursa zilizopo kwa kuanzisha vituo vya mafuta katika maeneo ya vijijini ili kusogeza huduma karibu na wananchi.

Na Mzidalfa Zaid

Mhina amesema kuwa uwekezaji katika vituo vya mafuta vijijini utarahisisha upatikanaji wa nishati, kuchochea shughuli za kiuchumi na kufungua fursa za ajira katika maeneo husika.

Sauti ya meneja wa EWURA kanda ya kaskazini

Aidha, amesisitiza kuwa wawekezaji wanapaswa kufuata taratibu na kanuni zinazowekwa na EWURA ili kuhakikisha vituo vinajengwa na kuendeshwa kwa kuzingatia viwango vya usalama na ubora wa huduma.