FM Manyara

TGNP yasaidia wakulima Manyara kupata uelewa wa kilimomisitu

12 June 2026, 7:26 pm

Baadhi ya wakulima wa kituo cha Taarifa na Maarifa Mamire wakifuatilia mafunzo ya Kilimomisitu

Mtandao wa Jinsia Tanzania TGNP kwa kushirikiana na baadhi ya wakulima kutoka vituo vya taarifa na maarifa  vya mamire na Murray mkoani Manyara wamefanya mafunzo ya pamoja ya nadharia na vitendo yanayohusu Kilimomisitu.

Akizungumza na Fm Manyara  Msimamizi wa mafunzo hayo ya siku nne yaliyofanyika katika kijiji cha Mamire Wilayani Babati Kutoka TGNP  Ester William amesema lengo la semina hiyo kwa wakulima hao ni kujifunza dhana ya Kilimo misitu na kanuni za kilimo Ikolojia pamoja na masuala ya Jinsia na kilimo himilivu kwa mabadiliko ya tabia nchi. 

Sauti ya Msimamizi wa mafunzo Kutoka TGNP  Ester William

Kwa upande wake mtaalamu wa Kilimomisitu anayefanya kazi na mtandao huo na mtoa mada kwenye mafunzo hayo Valence Kiangi  ameeleza sababu zinazopelekea kutokea kwa mabadiliko ya tabia nchi.

Sauti ya mtaalamu wa Kilimomisitu

Aidha afisa kilimo wa kata ya mamire Emanuel Lohaay Amebainisha faida zakufanya Kilimomisitu kwa wananchi huku akigusia kilimo hicho kama kitu ambacho kikitiliwa mkazo kinaweza kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi. 

Sauti ya afisa kilimo wa kata ya mamire

Nao baadhi ya washiriki katika semina hiyo ya Kilimomisitu wamekiri hawakuwahi kupatiwa mafunzo kama hayo hapo awali na kutoa pongezi kwa mtandao wa Jinsia Tanzania kwa kuona fursa hiyo kwa vituo hivyo vya taarifa na maarifa. 

Sauti ya baadhi ya washiriki katika semina ya Kilimomisitu

Mafunzo ya Kilimomisitu yamefanyika kwa nadharia na vitendo huku wakulima walioshiriki wakipata nafasi yakutengeneza mbolea ya asili iitwayo  Bokashi ambayo hutengenezwa bila kemikali kwa kutumia rasilimali zinazopatikana kwenye maeneo ya wakulima wanaofanya kilimo cha kutumia mbegu za asili. 

Mtaalamu wa kilimomisitu Valence Kiangi akifundisha jinsi ya kutengeneza Mbolea ya Bokashi