FM Manyara
FM Manyara
21 April 2026, 7:05 pm

Jamii mkoani Manyara imetakiwa kuachana Cha Imani potofu kuwa ugonjwa wa sikoseli unasababishwa kwa kulogwa au laana, bali ugonjwa huo unasababishwa kwa kurithi.
Na Mzidalfa Zaid
Hayo yameelezwa Leo na mratibu wa sikoseli na Hemofilia kutoka wizara ya afya dokta Astera Mpoto wakati wa mafunzo kwa waandishi wa habari mkoani Manyara kuhusu ugonjwa wa sikoseli na Hemofilia, ambapo amewataka waandishi wa habari kuelimisha jamii kuwa magonjwa hayo yanatokana kwa kurithi.
Kwa upande wake dokta bingwa wa watoto kutoka hospital ya rufaa ya mkoa wa Manyara dokta Joshua Girlabayda amesema katika mkoa wa Manyara watoto wenye ugonjwa wa sikoseli linazidi kuongezeka mwaka Hadi mwaka ambapo amesema katika hospital ya mkoa wa Manyara wanatibu watoto wenye tatizo hilo katika clinic za watoto.
Nae daktari bingwa wa magonjwa ya damu kutoka hospital ya Kanda ya Benjamin Mkapa Stella Malangahe, amesema wameanzisha huduma ya upandikizaji uloto kwa watoto wenye changamoto ya sikoseli ili kuisaidia kutoa matibabu sahihi ambapo mpaka Sasa watoto 30 wamepatiwa huduma hiyo.
Nao baadhi ya waandishi wa habari akiwemo afisa habari mkoa wa Manyara Ruth kyelula wamesema elimu ambayo wameipata wataifikisha kwa jamii ili kupata kuelewa kuhusu ugonjwa huo.
