Mpanda FM

Vijana washauriwa kuwa na maarifa kujiinua kiuchumi Katavi

8 September 2025, 2:49 pm

Baadhi ya vijana walioudhuria mjadala.picha na Anna Milanzi

wako tayari kufanya kazi ya kilimo na ufugaji ili waweze kujiinua kiuchumi

Na Anna Milanzi-Katavi

Vijana manispaa ya Mpanda mkoani Katavi wameshauriwa kuhakikisha wanakuwa na maarifa ili waweze kutunza fedha na kujikwamua kiuchumi.
Hayo yamejiri katika muendelezo wa mijadala ya vijana inayoandaliwa na mwandishi wa habari wa Mpanda Redio FM Anna Milanzi,ambapo vijana hao wameonesha kuhitaji Fedha zaidi kuliko kupata kwanza maarifa ya kuzitunza na nyenzo ya kuzalisha fedha.

Sauti za baadhi ya vijana manispaa ya Mpanda

Afisa maendeleo kutoka katika taasisi ya tuelimike Bavuga Sadock na mdau wa masuala ya kilimo na biashara ambae pia ni afisa kilimo John Kapesula wamezungumza na vijana hao na kuwaeleza umuhimu wa kuthamini fedha unayoipata kwa kufanya shughuli za kilimo, ufugaji na biashara ili kuindeleza fedha uliyonayo.

Sauti ya afisa maendeleo tuelimike na mdau wa kilimo na biashara
Vijana waliohudhuria mjadala wakiwa katika picha ya pamoja na mwandishi wa habari (wapili kulia )mdau wa kilimo na biashara (aliyevaa kijana )na afisa maendeleo kutoka taasisi ya tuelimike mwenye shati ya zambarau.

Kupitia elimu hiyo waliyoipata imebadilisha mtazamo kwa vijana hao huku wengi wao wakieleza kuwa wako tayari kufanya kazi ya kilimo na ufugaji ili waweze kujiinua kiuchumi kazi ambayo hapo awali hawakuona umuhimu wa kuifanya.

sauti za baadhi ya vijana walioshiriki mjadala

Kwa mujibu wa utafiti wa kilimo wa mwaka 2022/2023 uliofanywa na ofisi ya takwimu( NBS) na ofisi ya mtakwimu mkuu wa serikali (OCGS) kwa kushirikiana na wizara zinazoongoza sekta ya kilimo imeonesha kuwa sekta ya kilimo ni muhimu kwa ukuaji wa uchumi nchini,upatikanaji wa ajira,na kupunguza umasikini huku kilimo kikichangia asilimia 26.5 ya pato la taifa.