Mpanda FM

Longo: Wazazi, walezi wapatieni watoto haki ya elimu

16 July 2025, 4:04 pm

Afisa Ustawi wa Jamii Manispaa ya Mpanda Anyulumye Longo. Picha na Leah Kamala

“Usipompa mtoto haki yake ya elimu ni rahisi kujiingiza kwenye makundi hatarishi”

Na Leah Kamala

Baadhi ya wananchi wa manispaa ya Mpanda mkoani Katavi wametakiwa  kuwafundisha maadili mema watoto na kuwapatiwa haki yao ya elimu ili kujiepusha na makundi yasiyofaa.

Wakizungumza na Mpanda Radio FM kwa nyakati tofauti wananchi hao wamesema kuwa wanawajibika vyema kuhakikisha watoto wanapata elimu bora ili kuboresha maisha yao na jamii nzima.

Sauti za wazazi

Nae Afisa ustawi manispaa ya Mpanda mkoani Katavi Anyulumye Longo amewashauri wazazi na walezi kushirikiana na walimu na kutoa mahitaji muhimu ya shule kwa pamoja kwa ajili ya maendeleo ya watoto wao.

Sauti ya afisa ustawi

Elimu ni hazina kubwa kwa wanafunzi kwani huwajengea msingi wa maisha bora na  kutimiza ndoto zao ili kufikia mafanikio ya baadae.