Mpanda FM
Mpanda FM
16 April 2025, 1:29 pm

Picha ya mkuu wa wilaya ya Mpanda Jamila Yusuph. Picha na Anna Mhina
” Wazazi na walezi hakikisheni mnazingatia tarehe ya chanjo ya polio”
Na Edda Enock
Wazazi na walezi manispaa ya Mpanda mkoani Katavi wametakiwa kuzingatia kikamilifu chanjo kwa watoto ili kujikinga dhidi na ugonjwa wa polio.
Rai hiyo imetolewa na mkuu wa wilaya ya Mpanda Jamila Yusuph ambae alikuwa mwenyekiti katika kikao cha Taarifa ya utekelezaji wa lishe kwa nusu mwaka julai-Desember 2024 kwa mwaka wa Fedha 2024/2025.
Kwa upande wake mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Nsimbo Christina Bunini amewataka viongozi mbali mbali kuendelea kutoa Elimu juu ya umuhimu wa chanjo kwa wananchi hasa kwa wanawake wajawazito.
Nae Sophia Kumbuli mkurugenzi manispaa ya Mpanda amewataka viongozi kuhakikisha wanahamasisha wananchi kuhusiana lishe ,chanjo pamoja na usafi wa mazingira.
Kikao hicho kilikua kimelenga kutekeleza shughuli mbambali za lishe kwa lengo la kuimarisha afya na hali ya lishe katika jamii.