Mpanda FM
Mpanda FM
27 March 2026, 1:36 pm

“Tunaomba tupatiwe elimu maana hatuna uelewa”
Na Roda Elias
Wananchi wa Manispaa ya Mpanda mkoani Katavi wameomba kupatiwa elimu juu ya ugonjwa wa kipindu pindu kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha mkoani hapa ili kuepuka mlipuko wa ugonjwa huo.
Wakizungumza na Mpanda radio FM wananchi wamesema ugonjwa huo unasababishwa na mchafuko wa hewa, na mazingira kuwa machafu huku wakiiomba serikali kuwapatia elimu juu ya kujikinga na ugonjwa huo.
Kwa upande wake daktari Gabriel Elias ameeleza kuwa mara mtu anapopatwa ugonjwa huo dalili zake huanza kuonekana ndani ya siku mbili ,hivyo mgonjwa anapaswa kuwahishwa kituo cha afya kwa ajili ya matibabu.
Katika hatua nyingine Gabriel ameiasa jamii kuzingatia kanuni za afya ili kuepukana na kujikinga na ugonjwa huo.
Kwa mujibu wa European Centre for Disease Prevention and Control {ECDC} hadi kufikia Februari 2026 kumeripotiwa visa 25,000 na vifo 280 vilivyoripotiwa vya ugonjwa wa kipindupindu.