Mpanda FM

Hasara, madirisha 120 yapotea

27 February 2026, 4:41 pm

Mwenyekiti wa kikao cha kamati ya ushauri ya wilaya ya Mpanda ambaye pia ni DC wilaya ya Mpanda (aliye kati) akiwa na viongozi wengine.picha na Saga.

“Nimesikitishwa na uharibifu huu wa miundombinu, ulinzi ni lazima uwepo katika maeneo hayo”

Na Anna Milanzi-Katavi

Jumla ya madirisha 120 ya alminium yameibiwa  katika shule za msingi, sekondari pamoja na zahanati zilizopo manispaa ya Mpanda mkoani Katavi

Hayo yameelezwa wakati wa kuwasilisha rasimu ya bajeti ya mwaka 2026-2027 pamoja na kufanya mapitio ya bajeti zilizopita miaka ya fedha ya hivi karibuni kwa halmashauri ya Nsimbo pamoja na manispaa ya Mpanda ambapo kwa manispaa ya Mpanda Leonard Kilamhama ambaye ni mchumi manispaa ya Mpanda amewasilisha kwa niaba ya mkurugenzi wa manispaa ya Mpanda na kuainisha wizi huo.

Sauti ya Leonard Kilamhama ambaye ni mchumi manispaa ya Mpanda

Miongoni mwa wajumbe waliokowemo katika kikao hicho ni pamoja na Mbunge wa viti maalumu Mkoa wa Katavi Martha maliki, amesikitishwa na vitendo hivyo na kuomba ulinzi kuhimarishwa katika miundombinu.

Sauti ya mbunge wa viti maalumu Mkoa wa Katavi Martha maliki

Mwenyekiti wa kikao hicho ambaye ni mkuu wa wilaya ya Mpanda Jamila Yusuph ameielekeza kamati ya usalama kuchukua hatua zaidi juu ya jambo hilo.

Sauti ya wenyekiti wa kikao hicho ambaye ni mkuu wa wilaya ya Mpanda Jamila Yusuph
Mwenyekiti wa kikao, mkuu wa wilaya ya Mpanda Jamila Yusuph.picha na Saga

Kadhalika na hilo mkuu wa wilaya ya Mpanda Jamila Yusuph  amepongeza ongezeko la bajeti kwa kila halmashauri ambapo halmashauri ya wilaya ya Nsimbo  katika bajeti iliyopita ilikuwa ni billion 27.4  na kwasasa ni billion 35.7  huku manispaa ya Mpanda bajeti iliyopita ni Bilioni 33.9 kwa sasa ni Bilion 35.2 amesisitiza bajeti zote hizo zimelenga maendeleo kwa wananchi kama ambavyo serikali inasisitiza.