Mpanda FM
Mpanda FM
26 February 2026, 4:03 pm

“Msikubali kupitwa nafursa ya bima ya afya”
Na Betord Chove
Watu wapatao 23,236 kutoka kaya masikini wanatarajia kunufaika na huduma ya bima kwa afya kwa wote kupitia mfuko wa TASAF mkoani Katavi.
Akitoa taarifa wakati wa hafla ya uzinduzi wa bima ya afya kwa wote kwa wanaolipiwa na serikali mkoani Katavi Meneja wa NHIF Ally Mwakababu amesema Mpanda manispaa waliondikishwa ni 1560, Nsimbo 1774, Mpimbwe 1151, Mlele 303, Tanganyika 1172, huku changamoto kadhaa zikijitokeza wakati zoezi hilo likiendelea.
Mgeni Rasmi katika uzinduzi huo mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Hoza Mrindoko amewataka wanufaika wote wa awamu ya kwanza kuhakikisha wanasajiliwa ili waweze kunufaika na bima ya afya kwa wote.

Kwa upande wa wanufaika waliofanikiwa kujiandikisha na kupata bima hizo awamu ya kwanza wameishikuru serikali kwa kuwapa huduma hiyo ambayo awali ilikuwa changamoto kutokana na ugumu wa maisha.
Awamu ya kwanza ya uandikishaji wa bima ya afya kwa wote nchini inatarajiwa kuwasajili wanufaika milioni moja laki moja na ishirini na tano mia tatu thelathini {1,125330} ambao ni wazee, watoto , mama wajawazito, watu wenye ulemavu na watu wenye mahitaji maalumu waliotambuliwa na TASAF.
.