Mpanda FM
Mpanda FM
21 February 2026, 7:19 pm

Wanatumia vitambaa na wengine kutumia mikono pasipo kujua njia sahihi za kitaalamu kwa ajili ya kusafisha vinywa vya watoto.
Na Rhoda Elias-Katavi
Baadhi ya wananchi manispaa ya Mpanda mkoani Katavi wameeleza kuwa hawana uelewa wa kutosha juu ya namna sahihi ya kusafisha vinywa vya watoto walio na umri chini ya miaka 5
Wakizungumza na Mpanda Redio FM wananchi hao wamedai kuwa wengi wao wanatumia vitambaa na wengine kutumia mikono pasipo kujua njia sahihi za kitaalamu kwa ajili ya kusafisha vinywa vya watoto huku wakiiomba serikali kuwapa elimu.
Kwa upande wake mtaalam wa Afya ya kinywa na meno Kelvin Mlemi kutoka hospitali ya manispaa ya Mpanda ametaja njia sahihi za kusafisha kinywa cha mtoto.
Aidha mlemi amesema kuwa mtoto asiposafishwa kinywa chake kwa njia sahihi inapelekea harufu mbaya mdomoni na kutoa wito kwa jamii kutowapa watoto vyakula vilivyo na sukari kwa wingi ili kuepuka kuharibika kwa fizi
Afya ya kinywa kwa mtoto inaanza kipindi ambacho mtoto anaanza kuota jino moja na kuendelea hivyo mzazi anapaswa kuzingatia usafi wa kinywa cha mtoto.