Mpanda FM

Mtoto achomwa kisu cha moto, mama mzazi ahusika

19 February 2026, 2:22 pm

picha na Mwananchi

Amepata majeraha baada ya kuchomwa kisu cha moto na mama  yake mzazi kwa madai ya kuwa na tabia ya kuomba pesa kwa majirani

Na Rhoda Elias-Katavi

Mtoto  mmoja mwenye umri wa miaka 4 ambae ni mkazi wa mtaa wa Mpanda Hotel kata ya Mpanda Hotel katika Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi amepata majeraha baada ya kuchomwa kisu cha moto na mama  yake mzazi kwa madai ya kuwa na tabia ya kuomba pesa kwa majirani.

Wakizungumza na Mpanda redio FM jirani na ndugu wa karibu wa mtoto huyo wamedai kuwa mama wa mtoto  amekua na tabia zisizofaa za kuadhibu watoto wake kupita kiasi

Sauti ya majirani

Nae Dachi Dadesi ambae ni mwenyekiti wa kikundi cha kupinga ukatili na unyanyasaji wa kijinsia mkoani Katavi (SUMAUJATA) ametaja sababu za ukatili huo kuwa ni changamoto za kifamilia .

Sauti ya mwenyekiti wa kikundi cha kupinga ukatili na unyanyasaji wa kijinsia Katavi(SUMAUJATA)

Kwa upande wake mwenyekiti wa mtaa huo Ibrahim Msanda amekiri kuwepo kwa tukio hilo na tayari wamechukua hatua za kumpeleka mama huyo kituo cha polisi na kutoa  rai kwa wakazi wa mtaa huo kuripoti matukio ya ukatili  kwa ajili ya usalama wa watu wote.

Sauti ya mwenyekiti wa mtaa wa Mpanda hotel Ibrahim Msanda