Mpanda FM
Mpanda FM
3 February 2026, 3:30 pm

“Mtunze kila kitu mnachokikuta kuanzia majengo mpaka samani”
Na Samwel Mbugi
Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwananamvua Hoza Mrindoko amewataka wanafunzi na walimu wa shule ya Ufundi Mgombe secondary school iliyopo wilaya ya Mlele kijiji cha Uzega kutunza miundombinu ya shule hiyo.
Akizungumza mbele ya wanafunzi hao Mwanamvua amesema historia itakwenda kuandikwa kupitia wanafunzi ambao wamekuwa wa kwanza kuanza masoma katika shule hiyo.
Joseph Emmanuel Lugongo ni makamu mkuu wa shule ya Mgombe secondary school amesema wanafundisha masomo ya kumuwezesha mwanafunzi kuwa na ujuzi na maarifa kama vile ufundi magari na umeme.
Ikumbukwe kuwa kuanzishwa kwa shule za Ufundi ni maagizo ya Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan ili vijana waweze kutumia fursa hiyo kujiajiri.