Mpanda FM

Wanaobana mkojo hatarini figo kufeli

4 September 2025, 10:38 am

Mganga Mfawidhi wa kituo cha afya cha Town Clinic Dkt. Gabriel Elias. Picha na Anna Mhina

” Kukaa na mkojo kwa muda mrefu kunaweza kusababisha figo kushindwa kufanya kazi”

Na Anna Mhina

Wananchi wa Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda mkoani Katavi wametakiwa kuacha tabia ya kubana haja ndogo kwa muda mrefu (mkojo) ili kuepukana na madhara yanayoweza kujitokeza.

Akizungumza na Mpanda Radio FM, mganga mfawidhi wa kituo cha afya cha Town Clinic Gabriel Elias ameeleza madhara yatokanayo na kukaa na mkojo kwa muda mrefu ikiwemo U.T.I sugu pamoja na kusababisha figo kushindwa kufanya kazi ipasavyo.

Sauti ya Dkt. Gabriel

Baadhi ya wananchi wa Mpanda Hotel wameeleza sababu zinazosababisha kukaa na haja ndogo muda mrefu kuwa ni uvivu, matumizi ya simu, kujali biashara, ukosefu wa elimu juu ya madhara  ya kitendo hicho na hofu ya matumizi ya vyoo visivyo salama hasa maeneo ya biashara.

Sauti za wananchi

Kukaa na haja ndogo kwa muda mrefu kunachangia uwezekano wa kuunda mawe kwenye kibofu cha mkojo kutokana na mkusanyiko wa chumvichumvi zilizopo na kusababisha maumivu makali na kuziba kwa mirija hiyo .