Mpanda FM

CCM yaweka wazi majina ya wateuliwa watakaowania udiwani katika kata 58 Katavi

17 August 2025, 3:15 pm

Katibu wa siasa na uenezi CCM mkoa wa Katavi Teonas Kinyonto akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi za chama cha mapinduzi mkoa wa Katavi.picha na Anna Milanzi

kikao cha halmashauiri kuu kupitia chama cha mapinduzi CCM mkoa wa Katavi kilichofanyika August 13,2025 kimewateua wagombea udiwani katika kata hizo

Na Anna Milanzi-Katavi

Chama cha mapinduzi CCM mkoa wa Katavi kimeteua majina ya wagombea udiwani katika kata 58 zilizopo mkoani humo.

Akitangaza majina ya wagombea udiwani walioteuliwa August 17,2025 katika ofisi za chama cha mapinduzi mkoa wa Katavi  ,Katibu wa siasa na uenezi  CCM Teonas Kinyonto amesema kikao cha halmashauiri kuu kupitia chama cha mapinduzi CCM mkoa wa Katavi kilichofanyika August 13,2025 kimewateua wagombea udiwani katika kata hizo ili kupeperusha bendera ya chama hicho katika uchaguzi mkuu utakaofanyika  October 29,2025

Sauti ya Katibu wa siasa na uenezi CCM mkoa wa Katavi akitaja majina ya walioteuliwa

Katika wilaya ya Mpanda jimbo la Nsimbo pamoja na  manispaa ya mpanda jimbo la Mpanda amewataja pia walioteuliwa kuwania udiwani katika kata za  majimbo hayo huku baadhi ya majina yakiwa ni majina ya waliowahi kuwa madiwani katika kata hizo.

Sauti ya katibu wa siasa na uenezi CCM mkoa wa Katavi akiwataja walioteuliwa kuwania udiwani katika kata za majimbo mawili

Kupitia majina hayo yaliyosomwa yanaonyesha idadi ndogo ya wanawake watakaogombea udiwani kupitia chama hicho ambapo Kinyonto  amesema walipita kila mahali kuhamasisha wanachama wa chama hicho kujitokeza kushiriki katika mchakato huo wa uchaguzi.

Sauti ya katibu wa siasa na uenezi CCM Katavi Teonas Kinyonto akieleza hamasa waliyoitoa kwa wanachama wote kuchukua fomu ili kuwania nafasi hizo za udiwani

Kinyoto amewapongeza wanawake wote waliojitokeza katika mchakato wa kuchukua fomu na kugombea lakini pia amewapongeza  walioteuliwa kugombea udiwani katika kata zao.