Mpanda FM

“Wazazi, walezi zingatieni makuzi ya watoto”

14 July 2025, 2:16 pm

Afisa Maendeleo ya Jamii manispaa ya Mpanda Irene Samson. Picha na Samwel Mbugi

“Tunashindwa kujikwamua kiuchumi kwa sababu tunapenda starehe”

Na Anna Mhina

Wazazi na walezi mkoani Katavi wametakiwa kusimamia malezi na makuzi ya watoto wao ili kuwaepusha kujiunga na makundi yasiofaa.

Hayo yamesemwa na Irene Samson ambaye ni afisa maendeleo ya jamii manispaa ya Mpanda kufuatia baadhi ya vijana kushindwa kujikwamua kiuchumi kutokana na kutokuishi uhalisia wao.

Sauti ya afisa maendeleo ya jamii

Emmanuel Charles, Neema Nelson na Salum Haji ni baadhi ya vijana wa manispaa ya  Mpanda wameeleza sababu zinazopelekea kushindwa kujikwamua kiuchumi ikiwemo kuendekeza starehe na vitu vya anasa.

Sauti ya vijana

Hata hivyo mitandao ya Kijamii imekua ikitajwa kama chanzo cha baadhi ya vijana kuishi maisha yasiyo halisi na kusababisha kushindwa kuwajibika kiuchumi.