Mpanda FM

Msisite kutoa taarifa mnapofanyiwa ukatili

12 June 2025, 3:51 pm

Koplo Celsius Mlolele akitoa elimu ya ukatili wa kijinsia kwa wanafunzi. Picha na Samwel Mbugi

“Unafanyiwa ukatili nyumbani darasani unashindwa kuelewa”

Na Anna Mhina

Wanafunzi mkoani Katavi wametakiwa kutoa taarifa pindi wanapofanyiwa matukio ya ukatili wa kijinsia  ili waweze kutimiza malengo yao.

Hayo yamesemwa na afisa wa dawati la jinsia  wanawake na watoto wilaya ya Mpanda afande Veronica na koplo Celsius Mlolele wakati akitoa elimu katika shule ya sekondari Rungwa .

Sauti za maafisa wa dawati la jinsia na watoto

Kwa upande wao baadhi ya wanafunzi wa shule ya sekondari Rungwa na Mpanda Girls wameipokea kwa furaha elimu hiyo na kueleza namna watakavyotoa taarifa endapo wakiona viashiria vya matendo ya ukatili  wa kijinsia.

Sauti za wanafunzi

Akizungumza kwa niaba ya mkuu wa  shule ya sekondari Rungwa mwalimu Mackson Mapunda  amelipongeza dawati la jinsia kwa kufika shuleni hapo na kutoa elimu.

Sauti ya mwalimu

Utoaji wa elimu ya ukatili  wa kijinsia katika shule ya sekondari Rungwa ni mpango uliowekwa na  Mpanda redio FM katika kuelekea maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika june 16 mwaka huu.