Mpanda FM

Wafanyabiashara wakerwa na taka zitokanazo na karanga

19 May 2025, 4:22 pm

Takataka za maganda ya karanga eneo la Mpanda hotel

uchafu huo unaotokana na viwanda hivyo zinawasababisha wao kupata mafua ya mara kwa mara na kuharibu biashara zao

Na Samwel Mbugi-Katavi

Baadhi ya wafanyabiashara wa soko la jioni linalofanyika eneo la kata ya Mpanda hotel manispaa ya Mpanda mkoa wa Katavi wamelalamika kuhusu viwanda vya kubangulia karanga vilivyopo katika eneo hilo kusababisha vumbi linaloathiri biashara ya chakula.

Wameyasema hayo wakati wakizungumza na Mpanda Redio FM kuwa uchafu huo unaotokana na viwanda hivyo zinawasababisha wao kupata mafua ya mara kwa mara na kuharibu biashara zao hususani kwa wanaouza chakula.

Sauti ya wafanyabiashara Mpanda hotel

Kwa upande wake mwenyekiti  wa mtaa huo Ibrahim Msanda amesema kuwa eneo hilo ambalo linatumika kwa wafanyabiashara hao sio eneo la kudumu  na utaratibu wa kuwatafutia eneo lingine ambalo litakuwa rafiki unaendelea kufanyika.

Sauti ya mwenyekiti mtaa wa Mpanda Hotel Ibrahim Msanda

Ikumbukwe kuwa mwezi April mwaka huu mkuu wa wilaya ya Mpanda Jamila Yusuph alimtaka mkurugenzi  wa halmashauri ya manispaa ya Mpanda Sophia Kumbuli kuhakikisha taka hizo zinazolewa ndani ya siku saba, Hata hivyo jitihada za kumtafuta mkurugenzi zinaendelea ili kutolea ufafanuzi.