Mpanda FM

Uharibifu wa makazi ya watu wamuibua DC Jamila

19 May 2025, 3:30 pm

Mkuu wa wilaya ya Mpanda Jamila Yusuph

Miche hiyo itasaidia kupunguza ukame na madhara mengine yanayotokana na uharibifu wa mazingira

Na Ban Gadau -Katavi

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuph Kimaro amegawa miche ya miti zaidi ya laki moja kwa wakazi wa Kijiji cha mbugani kata ya kakese katika jitihada za kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi.

Akizungumza wakati wa ugawaji wa miche hiyo Jamila Yusuph amesema kuwa miti hiyo itasaidia kupunguza ukame na madhara mengine yanayotokana na uharibifu wa mazingira huku akitolea mfano wa tukio la hivi karibuni ambapo nyumba kadhaa ziliezuliwa na upepo mkali kutokana na uchache wa miti ya kutuliza upepo.

Sauti ya mkuu wa wilaya ya Mpanda Jamila Yusuph

Kwa upande wake afisa kutoka Wakala wa huduma za misitu Tanzania (TFS) Oswad Laswai ameendelea kuwahamasisha wananchi kuwa na muamko wa kupanda miti na kuitunza kwa ajili ya vizazi vijavyo.

Sauti ya afisa kutoka kwa wakala wa huduma za misitu Oswad Laswai

Nao baadhi ya wananchi mara baada ya kukabidhiwa miti hiyo wamemshukuru Mkuu wa wilaya kwa jitihada anazo endelea kuzionesha katika kukabiliana na Mabadiliko ya tabia nchi kwa kugawa miche hiyo kwa ajili ya ustawi wa kijiji chao na vizazi vijavyo.

Sauti za wananchi