Mpanda FM

Chadema Katavi wamtemea cheche Makalla

27 March 2025, 4:33 pm

Picha ya Katibu wa CHADEMA wilaya ya  Mpanda Richard Mponeja. Picha na Edda Enock

“Msimamo wetu ni kuhakikisha kuwa na uchaguzi huru, wa haki na usalama”

Na Edda Enock

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wilaya ya Mpanda mkoani Katavi  Kimetoa tamko  kwa kauli ya  Katibu Itikadi na Uenezi Na Mafunzo CCM Taifa Amos Makalla  ya CHADEMA kununua virusi vya Ebola na Mpox kwa lengo la kuzuia na kuhatarisha uchaguzi mkuu wa mwaka huu.

 Baadhi ya wanachama wa Chama hicho Wakizungumza na mpanda  Radio Fm wamesema kuwa kauli hiyo ya  kiongozi wa CCM ni uchochezi na jaribio la kupotosha umma na kuharibu sifa ya chama hicho.

Sauti ya wanachama

Kwa upande wake Katibu wa CHADEMA wilaya ya  Mpanda Richard Mponeja amesema  kuwa msimamo wao ni kuhakikisha kuwa na uchaguzi huru, wa haki na usalama, na watahakikisha haki ya kupiga kura inaheshimiwa kwa kila Mtanzania.

Sauti ya katibu

Ikumbukwe kiongozi huyo wa chama tawala nchini  alinukuliwa akitoa kauli hiyo  Machi 22 mwaka huu  wakati alipokuwa akizungumza na wanachama wa CCM, Mkoa wa Simiyu. 

Sauti ya Amos Makalla

Uchaguzi mkuu wa kuchagua viongozi mbalimbali unatarajiwa kufanyika Octoba 2025 nchini Tanzania.