Mpanda FM

Wafanyabiashara watakiwa kuchangamkia fursa

20 February 2025, 4:58 pm

Picha ya mwenyekiti wa shirikisho la umoja wa machinga, Haji Mponda. Picha na Samwel Mbugi.

“Jisajilini ili mkizi vigezo muweze kupata mkopo”

Na Samwel Mbugi

Wafanyabiashara wadogo wadogo maarufu kama Machinga wamehamasishwa kujitokeza kwa wingi   kuomba mikopo inayotolewa na serikali yenye riba ndogo  kupitia umoja wa shirikisho la wa machinga.

Hayo yamesemwa na mwenyekiti wa shirikisho hilo Haji Mponda ambapo amewataka wafanyabiashara wadogo wadogo  wote kuhakikisha wamejisajili ili kupata vitambulisho ili wakidhidi vigezo vya kupata mkopo huo.

Sauti ya mwenyekiti

Nae Peter Mwanansila katibu wa   shirikisho la la umoja wa wamachinga  wilaya ya Mpanda amesema kitambulisho cha machinga   kitamsaidia mjasirimali kufanya shughuli zake bila kubugudhiwa na  kupata  mkopo wenye riba nafuu.

Sauti ya katibu

Hata hivyo kuwa fomu kwa ajili  ya mkopo huo zinatolewa bila malipo yeyote kwa wajisiriamali wadogo wadogo.