Mpanda FM

Wananchi watakiwa kutunza mazingira

19 February 2025, 9:15 am

This image has an empty alt attribute; its file name is takawww-1024x756.jpg

Picha ikionesha takataka zilizotupwa ovyo. Picha na Leah Kamala

“Wananchi watunze mazingira ili kuepuka magonjwa ya mlipuko”

Baadhi ya wananchi wa manispaa ya Mpanda mkoani Katavi wameta maoni yao mseto kuhusiana na mandhara ya utupaji holela wa taka katika mazingira.

Wakizungumza na Mpanda radio FM kwa nyakati tofauti, wananchi hao wamesema kuwa utupaji holela wa taka husababisha uchafuzi wa mazingira pamoja na magonjwa ya mlipuko ikiwemo kipindupindu.

Sauti ya wananchi

Kwa upande wake afisa afya manispaa ya Mpanda mkoani Katavi Erick Kisaka amesema kuwa takataka zisipotunzwa vizuri husababisha madharia ya nzi na kufanya mazingira kuwa machafu, hivyo amewashauri wananchi kuchukua hatua ili kuepukana na magonjwa yanayotokana na utupaji wa taka.

Sauti ya afisa afya

Wananchi wanajukumu kubwa katika kuhakikisha usafi wa mazingira na kupambana na utupaji holela wa taka ili kupunguza changamoto ya magonjwa ya mlipuko.