Mpanda FM

Wananchi, viongozi Tanganyika watakiwa kushirikiana dhidi ya udumavu

13 February 2025, 11:47 am

Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika Onesmo Buswelu akiwa katika studio za Mpanda Redio FM

Wilaya ya Tanganyika kwa kushirikiana na sekta ya elimu, afya, kilimo na ufugaji  wanahakikisha wanasimamia mikakati itakayosaidia kutokomeza hali ya udumavu  kwa watoto.”

Na Rachel Ezekekia -Katavi

Wananchi halmashauri ya wilaya ya Tanganyika wametakiwa kushirikiana na viongozi wa serikali katika mpango wa kutokomeza hali ya udumavu katika wilaya hiyo .

Akizungumza na redio fm mkuu wa wilaya ya Tanganyika Onesmo buswelu amesema kuwa wilaya ya tanganyika kwa kushirikiana na sekta ya elimu, afya ,kilimo na ufugaji  wanahakikisha wanasimamia mikakati itakayosaidia kutokomeza hali ya udumavu  kwa watoto.

Sauti ya mkuu wa wilaya ya Tanganyika

Aidha  amebainisha mipango na mikakati ya wilaya Tanganyika inatekeleza katika kuhakikisha  wanaboresha  hali ya maendeleo na miradi mbalimbali kwa wananchi katika kipindi cha mwaka huu na miaka ijayo ikiwa ni pamoja na kuboresha hali ya miundombinu  kwa usatawi wa wananchi

Sauti ya mkuu wa wilaya ya Tanganyika

Katika hatua nyingine ameeleza juhudi za halimashauri ya wilaya ya Tnganyika ambazo zinafanywa kuhakikisha  kuna ushirikiano mzuri kati ya wananchi na vyombo vya usalama ili kuhakikisha  amani ulinzi pamoja na utulivu unadumishwa katika wilaya ya tanganyika.

Sauti ya mkuu wa wilaya ya Tanganyika akieleza juhudi zinazofanyika