Mpanda FM

Serikali yatoa mashine ya kifua kikuu Katavi

10 February 2025, 3:35 pm

Dr. Banuba Deogratias mganga mfawidhi hospitali ya Rufaa mko wa Katavi. Picha na Anna Mhina

“Wananchi wajitokeze kuchunguzwa vimelea vya kifua kikuu”

Wananchi  mkoani wa Katavi wametakiwa  kujitokeza ili kuchunguzwa vimelea vya ugonjwa wa kifua kikuu Kutokana na uwepo  wa mashine mpya za kuchunguza.

Akizungumza na Mpanda Radio FM  mganga mfawidhi wa hospitali ya Rufaa mkoa wa Katavi  Banuba Deogratias  amesema kutokana na vifaa tiba hivyo mgonjwa anachunguzwa na kuanza tiba mara baada ya kugundulika kuwa na vimelea vya kifua kikuu.

Mganga mfawidhi

Kwa upande wao baadhi ya wananchi wameishukuru serikali kwa hatua hiyo  ya kuleta mashine za uchunguzi wa vimelea vya kifua kikuu huku wakiiomba kupatiwa huduma ya vipimo bure  kutokana na kuwepo kwa gharama za matibabu.

Sauti ya wananchi

Haya yamejiri kufuatia hatua ya serikali katika jitihada za kudhibiti na kutokomeza ugonjwa wa kifua kikuu (TB) kwa  kugawa mashine mpya 185 zenye thamani ya sh. billion 7 kwa ajili ya uchunguzi na ugunduzi wa vimelea vya ugonjwa huo nchini.