Mpanda FM

Wananchi washauriwa kutumia mahakama kwa njia ya mtandao

7 February 2025, 12:18 pm

Picha ya hakimu mkazi mfawidhi Gway Sumaye. Picha na Anna Mhina

“Wananchi watumie mahakama kwa njia ya mtandao ili kuokoa pesa”

Na Lilian Vicent

Wananchi mkoani Katavi wameshauriwa kutumia mahakama kwa njia ya mtandao ili kuokoa muda pamoja fedha zitakazotumika kufutilia madai ya kesi zao.

Akizungumza na Mpanda redio FM hakimu mkazi mfawidhi wa mahakama ya hakimu mkazi mkoa wa Katavi Gway Sumaye amebainisha  kupitia njia hiyo wameweza kuokoa pesa nyingi.

Sauti ya hakimu mkazi mfawidhi

Sumaye ameongeza kuwa kwa wananchi ambao hawatumii simu janja wanatakiwa kwenda kwenye mahakama za wilaya zilizopo katika maeneo yao kwa ajili kushughulikiwa kesi zao.

Sauti ya hakimu mkazi mfawidhi

Kwa upande wako   baadhi ya wananchi wamesema usikilizwaji wa kesi kwa njia ya mtandao utawasaidia watu wanaoishi mbali na mahakama kupata haki zao.

Sauti ya wananchi

Kwa mujibu wa  hakimu mkazi mfawidhi amesema  takwimu  kwa mwaka 2024 kesi 30 na kuendelea zikihusisha kesi za mahabusu  zilisikilizwa kwa njia ya mtandao.