Mpanda FM

Takukuru Katavi yaokoa 120,300,000

27 January 2025, 5:30 pm

Picha ya Stuart Kiondo akizungumza na waandishi wa habari. Picha na Lilian Vicent

“Stendi kuu ya Mizengo Pinda  kuna mapungufu katika ukusanyaji wa mapato”.

Na Lilian Vicent

Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa (TAKUKURU) mkoa wa Katavi imefanikiwa kuokoa fedha kiasi cha shilingi milioni  mia moja ishirini na laki tatu (120,300,000) ambazo zilikuwa zitumike vibaya katika utekelezaji wa miradi mbalimbali kwa robo ya pili iliyoanza oktoba hadi disemba 2024.

Hayo yamesemwa na Kaimu mkuu wa TAKUKURU  mkoa wa Katavi Stuart Kiondo wakati akizungumza na vyombo vya habari ambapo  amesema shilingi milioni tisini na moja zimeokolewa za chama cha msingi ILANGU –AMCOS wilaya ya Tanganyika.

Sauti ya Stuart Kiondo

Aidha amebainisha  kuwa taasisi hiyo imefuatilia utekelezaji wa miradi  ishirini na saba 27  ya maendeleo yenye thamani  ya shilingi bilioni 7.6 katika sekta za elimu ,afya ,ulinzi na usalama na maendeleo ya jamii.

Sauti ya Stuart Kiondo

Katika hatua nyingine ameongeza kuwa  katika uchambuzi wa mifumo kwenye halmashauri ya Manispaa ya Mpanda  wamebaini katika mfumo wa ukusanyaji wa mapato ya stendi kuu ya mizengo Pinda  kuna mapungufu yanayopelekea kupoteza fedha nyingi.

Sauti ya Stuart Kiondo

Sanjari na hayo Kiondo amesema mikakati kwa kipindi cha Januari hadi Marchi imejipanga  kuzuia rushwa, kuendelea kuelimisha wananchi kuhusu madhara ya rushwa  tunapoelekea uchaguzi mkuu wa 2025  na kufanya uchunguzi.