Mpanda FM

Katavi : ACT wazalendo waja na mikakati kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa

24 September 2024, 8:24 pm

picha na mtandao

“Tunatakiwa kujipanga kwa ajili ya kushiriki na kuwania nafasi mbalimbali katika uchaguzi wa serikali za mitaa “

Na Lilian Vicent -Katavi

Baadhi ya wanachama wa Chama  cha ACT wazalendo mkoani katavi  wamesema kuwa wamejiandaa kushiriki uchaguzi  wa serikali za mitaa na uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 .

 Wameyasema hayo wakati wa  mahojiano na Mpanda redio FM katika ofisi za chama hicho  zilizopo manispaa ya Mpanda mkoani Katavi.

Sauti za wanachama wa chama cha ACT wazalendo

Kwa upande wake mwenyekiti wa chama hicho Joseph Mona amesema kwa mujibu wa taarifa za awali wametakiwa kujipanga kwa ajili ya uchaguzi    licha ya kesi iliyofunguliwa na viongozi wao  dhidi ya TAMISEMI .

Sauti ya mwenyekiti wa chama hicho Joseph Mona

Ikumbukwe kuwa August 25,2024 Chama hicho kilisema kimejiandaa vyema kushiriki Uchaguzi huo na wameshapeleka  kesi Mahakamani kuzuia TAMISEMI ambayo ni Wizara ya Serikali kusimamia Uchaguzi wa Serikali za Mitaa.