Mpanda FM

Katavi: Wafanyabiashara wa samaki watia neno kufunguliwa Ziwa Tanganyika

14 August 2024, 10:59 pm

picha na mtandao

“wanasubiri maelekezo ya waziri mwenye dhamana  na sekta hiyo  kuhusu ufunguzi wa ziwa Tanganyika na wanachi wataendelea na shughuli zao za uvuvi kama ilivyokuwa hapo awali.”

Na Lilian Vicent- Katavi

Baadhi ya wafanyabiashara na wanunuzi wa samaki manispaa ya  Mpanda mkoani Katavi wameeleza mapokezi yao kufuatia ufunguzi wa ziwa  Tanganyika linalotarajiwa kufunguliwa  Agosti 15,2024 .

Wameyasema hayo walipokuwa wanazungumza na Mpanda radio FM na kueleza kuwa  wakisubiri kwa muda mrefu ufunguzi wa ziwa hilo kwani   hali ya kibiashara imekuwa ngumu kutokana na uchache wa samaki.

 Sauti ya wananchi wakizungumza

Nehemia James ni Katibu tawala msaidizi  sehemu ya uchumi na uzalishaji  amesema kuwa    wanasubiri maelekezo ya waziri mwenye dhamana  na sekta hiyo  kuhusu ufunguzi wa ziwa Tanganyika na wanachi wataendelea na shughuli zao za uvuvi kama ilivyokuwa hapo awali.

Sauti ya Nehemia James ni Katibu tawala msaidizi  sehemu ya uchumi na uzalishaji

Ametoa rai kwa wananchi pindi tu shughuli za uvuvi zitapoanza zitafanyika kwa mujibu wa kanuni ,na taratibu kwaajili  kupambana na uvuvi haramu na kuwalinda samaki.

Sauti ya Nehemia James ni Katibu tawala msaidizi  sehemu ya uchumi na uzalishaji

Ikumbukwe kuwa Serikali kupitia wizara ya mifugo na uvuvi  ilifunga shughuli za uvuvi katika Ziwa Tanganyika tarehe 15 mwezi may mwaka huu  kwa lengo la kupumzisha ziwa hilo ili kuwezesha samaki kuzaliana na kuongeza tija kwa wavuvi wanaofanya shughuli zao ziwani humo.