Mpanda FM

RC Katavi awataka wataalam wa afya kutoa huduma bora

14 August 2024, 10:16 pm

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko wa pili kulia akiwa katika picha ya pamoja na viongozi mbalimbali. Picha na John Mwasomola

Serikali kuleta vifaa tiba kunasaidia kuboresha huduma katika sekta ya afya

Na John Mwasomola- Katavi

Wataalam wa afya wametakiwa kutumia weledi wao na ujuzi walionao katika kuendelea kutoa huduma bora za matibabu kwa wananchi mkoani Katavi.

Agizo hilo linakuja kufuatia vifaa vya kitaalam ambavyo vinaendelea kutolewa katika hospitali mkoani hapa .

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko katika hospital ya Rufaa ya Mkoa wakati wa hafla ya ugawaji wa vifaa vya kupima  saratani ya mlango wa shingo ya kizazi .

Aidha amewataka wataalamu hao kuvitunza vifaa hivyo na kuvifanyia matengenezo ya mara kwa mara kulingana na mkataba wake.

Sauti ya Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko akizungumza

Pia amewataka wanawake kujitokeza Kwenda kufanyiwa utafiti na vipimo ili kujua dalili au tatizo la saratani ya mlango wa shingo ya kizazi, ambapo huduma hizo zinapatikana katika Mkoa wa Katavi tofauti na hapo awali huduma hizo zilikua zinapatikana mikoa ya Jirani.

Sauti ya mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko

Kwa upande wake Kaimu mganga mfawidhi hospital ya rufaa Dkt. Frank Elisha amewashukuru wadau wa afya na serikali, kwa kuwaletea vifaa hivyo ambavyo vinakwenda kuleta sura mpya ndani ya Mkoa na kuahidi kuvitumia kama ilivyokusudiwa.

 Kaimu Mganga Mfawidhi Hospital ya Rufaa Dkt. Frank Elisha akizungumza

Rose Silvanus  ni mwananchi mkoani hapa ameelezea jinsi ilivyokua changamoto  hapo awali ya upatikanaji wa huduma za uchunguzi wa  saratani ya mlango wa  shingo ya kizazi  .

Sauti ya Rose Silvanus mwananchi mkoani Katavi

Tukio la kukabidhi vifaa vya kupima mlango wa kizazi kwa wanawake limefanyika katika Hospital ya Mkoa wa Katavi na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali, ambapo zoezi hilo limeongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko.