Mpanda FM

RC Mrindoko :Hospitali zinazodaiwa na MSD zilipe madeni

23 May 2024, 10:57 am

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko.Picha na Anna Milanzi

kulipa madeni katika hospitali ambazo zinadaiwa kutaongeza ufanisi katika utendaji kazi

Na Rachel Ezekia-Katavi

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Hoza Mrindoko amezitaka hospitali zinazodaiwa na bohari ya dawa kanda ya magharibi kulipa madeni yote ili  kurahisisha utendaji kazi wa bohari ya dawa (MSD) kutoa huduma zao kwa  ufanisi .

Mrindoko ameyasema hayo katika kikao kazi cha wadau wa bohari ya dawa kanda ya magharibi mkoa wa Katavi siku za hivi karibuni  ambapo  lengo  kuu  ilikuwa ni  kuhamasisha utendaji kazi bora .

Sauti ya mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko

Aidha amewataka bohari ya dawa (MSD) kutoa huduma za dawa katika vituo husika pindi ambapo madeni pamoja na ununuzi wa vifaa  kuhakikisha wanazingatia muda ili kutekeleza kazi na maono ya serikali .

Sauti ya mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko

Kwa upande wake Saraphine Patrice  mganga mfawidhi hospitali ya rufaa Katavi amesema wataalamu wa maabara wanafanya kazi kulingana na vitendea kazi pamoja na uwepo wa kutosha wa wataalamu wa dawa na taasisi kutoa ajira za mkataba kulingana na miongozo ya serikali kwa wataalum wa dawa.

Sauti ya mganga mfawidhi Saraphine Patrice