Mpanda FM
Mpanda FM
29 August 2023, 10:12 am
MPANDA Wanafunzi wa kidato cha tano na sita katika shule ya Sekondari ya Wasichana Mpanda wamesisitizwa kusoma kwa bidii ili kufikia ndoto zao. Msisitizo huo umetolewa na Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheli Tanzania (KKKT) Dayosisi ziwa Tanganyika (Rukwa/Katavi)…
29 August 2023, 10:05 am
TANGANYIKA. Baadhi ya Wananchi Mkoani Katavi wanaotumia Barabara ya Kabungu kwenda Karema wamelalamikia ubovu wa miundombinu ya barabara hiyo na kuitaka serikali kuifanyia matengenezo kwa kiwango cha lami. Wakizungumza na mpanda redio fm kwa nyakati tofauti wananchi hao wameleeza kuwa…
25 August 2023, 10:25 am
KATAVI Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa TAKUKURU mkoa wa Katavi imewafikisha mahakamani watumishi wa serikali 7 kwa makosa matatu ikiwemo wizi wa fedha zaidi ya bilioni 1.2. Kelvin Mwaja ni mwanasheria kutoka taasisi ya kuzuia na kupambana na…
24 August 2023, 8:39 am
MPANDA Baadhi ya wakulima katika kata ya Kasokola halmashauri ya manispaa ya Mpanda mkoani Katavi wamelalamikia wafugaji kulisha mifugo kwenye mazao yao hali ambayo inawarudisha nyuma kiuchumi. Wamebainisha hayo katika mkutano wa hadhara mbele ya mkuu wa wilaya ya Mpanda…
20 August 2023, 3:06 pm
MPANDA Wananchi wa mtaa wa Edeni kata ya Misukumilo halmashauri ya manispaa ya Mpanda mkoani Katavi wamemshuru Mbunge wa jimbo la Mpanda mjini Sebastian Kapufi kwa kuwapambania haraka kupata huduma ya maji safi na salama. Hayo yanajiri kufuatia ziara ya…
20 August 2023, 3:02 pm
NSIMBO Wakulima wa zao la tumbaku halmashauri ya Nsimbo mkoani Katavi wameutaka uongozi wa kampuni ya ununuaji wa tumbaku ya Mkwawa kuharakisha kufanya malipo ya zao hilo. Wakizungumza na kituo hiki kwa nyakati tofauti wakulima hao wametaja kuwa ucheleweshwaji wa…
18 August 2023, 10:18 am
Kufuatia mafunzo ya ujasiriamali yaliyotolewa na Mpanda Radio fm kwa kushirikiana na Mkwawa Vocation Training Center washiriki wa mafunzo hayo wamekiri mafunzo hayo yatawainua kiuchumi. Wameyasema hayo mara baada ya kutamatika kwa mafunzo hayo Agosti 17, 2023 na kubainisha namna…
18 August 2023, 10:06 am
MPANDA Wananchi wa kitongoji cha Bwawani mtaa wa Kigamboni wanaoishi pembezoni mwa bwawa la Milala mkoani Katavi wamelalamikia ucheleweshwaji wa fidia na taarifa kuhusu makazi yao, ambayo walisimamishwa kufanya shughuli zote za kimaendeleo. Wakizungumza na Mpanda Radio fm wananchi hao…
16 August 2023, 10:09 am
TANGANYIKA Mwenge wa uhuru unatarajia kuzindua na kutembelea miradi saba yenye thamani zaidi ya bilioni 1.9 katika wilaya ya Tanganyika mkoani Katavi Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake mkuu wa wilaya ya Tanganyika Onesmo Buswelu amebainisha kuwa mwenge wa…
16 August 2023, 7:16 am
Wananchi Mkoani Katavi waanza kunufaika na mafunzo ya Ujasiriamali yanayoendeshwa na Mpanda Radio FM kwa kushirikiana na Mkwawa Vocational Training Center, Mafunzo hayo yatatolewa Kwa siku tatu kuanzia August 15 Hadi August 17. #mpandaradiofm.97.0
Umiliki wa redio
Mpanda Radio FM inamilikiwa na kampuni iliyosajiliwa iitwayo Mpanda radio FM Limited na cheti cha usajili namba 78298 na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mpanda Radio FM pia imesajiliwa na Mamlaka ya Udhibiti wa Mawasiliano Tanzania TCRA, Wizara ya Viwanda na biashara; ama tunatambuliwa na Chama cha Wafanyabiashara, Viwanda na Kilimo Tanzania TCCIA na Mamlaka ya Mapato ya Tanzania kama Mlipa Ushuru, tuna Namba ya Kitambulisho cha Mlipa kodi 115-577-239 na tumepewa nambari ya usajili ya VAT 40-015708 kwa Biashara iliyoko hoteli ya Mpanda, eneo la eneo. nambari G, nambari ya kuzuia 35.
Dira
Kuwa jamii thabiti yenye afya bora, elimu, umoja na maendeleo endelevu, inayotambua wajibu na haki.
Dhamira
Kushirikisha jamii katika kuandaa vipindi, habari na uendeshaji wa redio kwa kuzingatia taaluma. Kuwa jukwaa la mijadala inayochochea mabadiliko chanya ya fikra, usawa wa jinsia, sheria na utawala bora, uwajibikaji, ushindani wa maendeleo, utamaduni na ulinzi wa rasilimali.
Uongozi
Mpanda Radio FM ina mlolongo mzuri wa uongozi na inasimamiwa na Bodi ya wakurugenzi. Tuna wakurugenzi watatu kwa hisa na kuajiriwa; pia tuna uongozi wa uzalishaji na uuzaji.
