Mpanda FM
Mpanda FM
9 October 2023, 12:37 pm
MpimbweMamlaka ya Mapato Tanzania TRA Mkoa wa Katavi imetoa elimu ya mabadiliko ya sheria mpya za kodi kwa wafanyabiashara wa halmashauri ya Mpimbwe pamoja na kusikiliza kero na kuzipatia ufumbuzi. Akizungumzia utoaji wa elimu hiyo Meneja wa TRA mkoa wa…
5 October 2023, 2:01 pm
Wananchi wa kijiji cha Magogo kata Kasekese wilaya ya Tanganyika mkoani Katavi wameishukuru serikali kwa kuwajengea shule kijijini hapo. Na Gladness Richard – Tanganyika Wananchi wa kijiji cha Magogo kata Kasekese wilaya ya Tanganyika mkoani hapa wameishukuru serikali kwa kuwajengea…
5 October 2023, 1:41 pm
Katibu mkuu wa Chama Cha mapinduzi taifa Daniel chongolo ameahidi kufanyia kazi mradi wa umeme wa gridi ya taifa Na John Benjamin – Mpanda Katibu mkuu wa Chama Cha mapinduzi ccm taifa Daniel chongolo ameahidi kufanyia kazi kuhakikisha mradi wa…
4 October 2023, 2:42 pm
Walimu wa shule za msingi manispaa ya Mpanda mkoani Katavi wameutaka uongozi wa mkoa kutolea ufafanuzi malalamiko ya kushindwa kupandishwa madaraja kwa muda mrefu. Na Ben Gadau – Mpanda KATAVIWalimu wa shule za msingi manispaa ya Mpanda mkoani Katavi wameutaka…
4 October 2023, 1:43 pm
Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Katavi kupitia CCM Taska Restituta Mbogo ametoa zaidi ya shilingi milioni tatu kwa ukamilishaji wa ofisi za CCM wilaya ya Mlele na ofisi ya UWT wilayani hapo. Na Ben Gadau – MleleMbunge wa Viti Maalumu…
2 October 2023, 10:11 pm
KATAVIKatibu mkuu wa chama cha mapinduzi CCM taifa Daniel Chongolo Amewasili Mkoani Katavi kuanza Ziara ya Siku 6 kwa ajili ya kukagua miradi na kuzungumza na wananchi. Kwa mujibu wa Taarifa iliyotolewa na chama cha Mapinduzi mkoani Katavi mara baada…
1 October 2023, 6:35 pm
TRA mkoa wa Katavi imewataka wananchi mkoani hapa ikiwemo wafanyabiashara na wanunuzi kuwa na utaratibu wa kutoa na kudai risiti KATAVI. Mamlaka ya mapato mkoa wa Katavi imewataka wananchi mkoani hapa ikiwemo wafanyabiashara na wanunuzi kuwa na utaratibu wa kutoa…
1 October 2023, 6:26 pm
Wananchi mkoani Katavi wametakiwa kuelewa sababu zinazo sababisha tatizo la kansa ya matiti Katavi Wananchi mkoani Katavi wametakiwa kuelewa sababu zinazosababisha tatizo la kansa ya matiti kwa wanawake ili kupata ufumbuzi wa haraka kipindi dalili zinapojitokeza. Mganga Mkuu manispaa ya…
1 October 2023, 6:00 pm
Wazazi na walezi wa Kagunga kata ya Kasekese wilayani Tanganyika wameshauriwa kuunda kamati ya chakula. TANGANYIKAWazazi na walezi wa kijiji cha Kagunga kata ya Kasekese wilayani Tanganyika mkoani Katavi wameshauriwa kuunda kamati ya chakula kwa ajili ya mwaka mpya wa…
1 October 2023, 5:47 pm
Madereva wa magari ya abiria na binafsi mkoani Katavi wametakiwa kuwa makini na kuchukua tahadhari katika kuelekea msimu wa mvua za masika KATAVI.Madereva wa magari ya abiria na binafsi mkoani Katavi wametakiwa kuwa makini na kuchukua tahadhari katika kuelekea msimu…
Umiliki wa redio
Mpanda Radio FM inamilikiwa na kampuni iliyosajiliwa iitwayo Mpanda radio FM Limited na cheti cha usajili namba 78298 na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mpanda Radio FM pia imesajiliwa na Mamlaka ya Udhibiti wa Mawasiliano Tanzania TCRA, Wizara ya Viwanda na biashara; ama tunatambuliwa na Chama cha Wafanyabiashara, Viwanda na Kilimo Tanzania TCCIA na Mamlaka ya Mapato ya Tanzania kama Mlipa Ushuru, tuna Namba ya Kitambulisho cha Mlipa kodi 115-577-239 na tumepewa nambari ya usajili ya VAT 40-015708 kwa Biashara iliyoko hoteli ya Mpanda, eneo la eneo. nambari G, nambari ya kuzuia 35.
Dira
Kuwa jamii thabiti yenye afya bora, elimu, umoja na maendeleo endelevu, inayotambua wajibu na haki.
Dhamira
Kushirikisha jamii katika kuandaa vipindi, habari na uendeshaji wa redio kwa kuzingatia taaluma. Kuwa jukwaa la mijadala inayochochea mabadiliko chanya ya fikra, usawa wa jinsia, sheria na utawala bora, uwajibikaji, ushindani wa maendeleo, utamaduni na ulinzi wa rasilimali.
Uongozi
Mpanda Radio FM ina mlolongo mzuri wa uongozi na inasimamiwa na Bodi ya wakurugenzi. Tuna wakurugenzi watatu kwa hisa na kuajiriwa; pia tuna uongozi wa uzalishaji na uuzaji.
