Mpanda FM

DC Buswelu akerwa na uzembe wa watumishi wa afya

1 April 2026, 9:49 am

Onesmo Buswelu mkuu wa wilaya ya Tanganyika. Picha na Anna Mhina

“Lazima tujirekebishe tufanye kazi kwa huruma na upendo”

Na Betord Chove

Mkuu wa wilaya ya Tanganyika Onesmo Buswelu ameonesha kutoridhishwa na hali ya uzembe kwa baadhi ya watumishi katika vituo vya afya wilayani humo akiwataka kujitathmini katika utekelezaji wa majukumu yao.
Akizungumza wakati wa ziara ya kukagua huduma za afya na kutembelea vituo vya afya vya Karema, Kasekese pamoja na zahanati ya Ikola,  Buswelu amesema kumekuwa na malalamiko makubwa kutoka kwa wananchi kuhusu utoaji wa huduma hali inayohitaji hatua za haraka kurekebishwa.

Sauti ya mkuu wa wilaya

Amesisitiza kuwa uzembe wa watumishi haupaswi kuwa sababu ya kuwaumiza wananchi akionya kuwa vitendo hivyo vinaharibu taswira ya serikali kwa wananchi.

Sauti ya mkuu wa wilaya

Katika hatua nyingine Buswelu amesema serikali haitavumilia kuona vifo vinavyoweza kuzuilika hususani vya wajawazito akitaka watumishi kuwajibika kikamilifu ili kuhakikisha huduma bora za afya zinapatikana kwa wananchi wote wa wilaya ya Tanganyika.