Mpanda FM
Mpanda FM
23 March 2026, 3:19 pm

“Lengo letu ni kuhakikisha amani na utulivu vinakuwepo katika mkoa wetu”
Na Samwel Mbugi
Sheikh mkuu wa mkoa wa Katavi Nassoro Kakulukulu ameendelea kuhimiza amani na mashirikiano baina ya dini zote katika kuhakikisha wanaihubili amani ya nchi ya Tanzania.
Akizungumza katika baraza la idd lililofanyika katika ukumbi wa manispaa ya Mpanda amesema lengo la mashirikiano na taasisi za dini ni kuhakikisha amani na utulivu vinaendelea kutawala kwa mkoa wa Katavi na Tanzania kwa ujumla.
Kwa upande wa mchungaji Enduru Masumo ametoa shukurani kwa umoja na msikamano kwa sheikh mkuu kwa kuendelea kuonyesha ushirikiano na dini zote jambo ambalo ameahidi kuonesha mshikamano huo.
Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Mpanda Jamila Yusuph akimwakilisha mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Hoza Mrondoko amesema wanatambua mchango unaotolewa na taasisi za dini katika kuwahudumia wananchi.
Hata hivyo Jamilia ametoa wito kwa wananchi wa mkoa wa katavi kuendelea kuwa na mshikamano katika kuhakikisha amani inaendelea kuwepo.