Mpanda FM
Mpanda FM
6 March 2026, 3:34 pm

Katibu mwenenzi akimkabidhi mwalimu kompyuta hizo. Picha na Betord Chove
“Walitupatia changamoto nyingi”
Na Betord Chove
Katibu mwenezi wa chama cha Mapinduzi (CCM) Kata ya Nsemulwa wilayani Mpanda mkoani Katavi Geofrey Alfonce Kipeta amekabidhi kompyuta mbili za mezani kwa shule ya sekondari Lyamba.
Akizungumza wakati wa halfa ya kukabidhi vifaa hivyo, Kipeta amesema amepeleka vifaa hivyo kufuatia ziara aliyofanya tarehe 3 mwezi wa 2 iliyokua na lengo la kutambua changamoto mbalimbali zinazoikabili shule hiyo.
Awali akisoma risala wakati wa makabidhiano hayo mkuu wa shule ya Sekondari Lyamba Josylin N. Myango amesema ujio wa kompyuta hizo utakwenda kuongeza ufaulu wa wanafunzi kutokana na changamoto mbalimbali za vifaa zilizokuepo katika shule hiyo.
Cyspin Myango mwenyekiti wa bodi ya shule na kaka mkuu wa shule hiyo wakizungumza kwa niaba ya wazazi na wanafunzi wametoa shukurani kwa mdau huyo wa elimu kwa mchango huo na kumwomba kutatua changamoto nyingine zinazowakabili ikiwemo Kichapishi.
Kwa mujibu wa mkuu wa shule hiyo , sekondari ya Lyamba imeanzishwa mwaka 2022 ikiwa na wanafunzi 246 kwa sasa ina wanafunzi 980 huku wakikabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo madawati, Kichapishi na Kiangazishi.