Mpanda FM
Mpanda FM
2 March 2026, 3:48 pm

Madiwani wakiwa kwenye kikao cha pili cha baraza. Picha na Samwel Mbugi
“Sasa mimi nisipokuwa na mia tatu ina maana nibaki”
Na Samwel Mbugi
Baraza la madiwani manispaa ya Mpanda mkoani Katavi limepiga marufuku matumizi ya tiketi za mkono zinazotumiwa na maajenti wa stendi ya kuu ya mabasi Mizengo Pinda kutokana na changamoto ya usumbufu wanaopata abiria ndani ya stendi hiyo.
Hayo yamejiri katika mkutano wa pili wa baraza la madiwani kwa mwaka wa fedha 2025/2026 uliofanyika kwenye ukumbi wa ofisi ya mkurugenzi baada ya madiwani kuhoji kuhusu ushuru wa sh. 300 unaotolewa mlangoni ukiwa na tiketi iliyoandikwa kwa mkono.
Kupitia kikao hicho mbunge wa jimbo la Mpanda mjini Haidary Hemed Sumry amekitaka kiti cha mwenyekiti wa kikao hicho ambae ni meya wa manispaa ya Mpanda kutoa msimamo baada ya kuona hakuna sababu za msingi kuwepo kwa tiketi hizo.
Mstahiki meya wa manispaa ya Mpanda Charles Philipo amesema atakaebainika anatoa tiketi ya mkono atachukuliwa hatua za kisheria ili iwe fundisho na wengine.
Ikumbukwe kuwa mwaka jana mkuu wa mkoa wa Katavi alitembelea stendi hiyo kwajili ya kusikiliza kero za wasafiri na miongoni mwa kero ilikuwa ni hiyo ambayo alitoa maagizo kwa mkurugenzi wa manispaa ya Mpanda kulifuatilia hilo kama lina umuhimu wa kutozwa abilia sh. 300 pindi anapoingia stendi.