Mpanda FM

Karema yakosa mawasiliano

26 February 2026, 3:37 pm

Daraja lililovunjika na kusababisha kukosekana kwa mawasiliano. Picha na Betord Chove

“Hakuna mtanzania anayeweza kuingia Karema”

Na Betord Chove

Daraja linalounganisha vijiji vya Ikola, Karema na makao makuu ya Wilaya ya Tanganyika mkoani Katavi limekatika kutokana na mvua  zinazoendelea kunyesha.

Baadhi ya wananchi wamesema wanalazimika kuvuka mto kwa kutumia mtumbwi, ambao hulipia shilingi 1,000, jambo linaloongeza ugumu wa maisha yao ya kila siku.

Sauti za wananchi

Kaimu Meneja wa Mamlaka ya barabara (TANROADS) Mkoa wa Katavi, Mhandisi Albert Laizer, amesema kazi ya kurejesha mawasiliano ya barabara hiyo tayari imeanza ili usafiri urejee kawaida.

Sauti ya meneja TANROADS

Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Mwanamvua Mrindoko, ameagiza Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) kufanya kazi usiku na mchana ili barabara kutoka Tanganyika kuelekea Bandari ya Karema irejee utendaji wake wa kawaida haraka.

Sauti ya mkuu wa mkoa

Aidha, amemuagiza Kamanda wa Kikosi cha Uokoaji kupeleka boti maalumu kuvusha wananchi salama na kupiga marufuku matumizi ya mitumbwi hatarishi.

Sauti ya mkuu wa mkoa