Mpanda FM
Mpanda FM
25 February 2026, 11:05 am

“Nilimtuma mdogo wake hakumkuta,tukaenda wote kumtafuta hadi usiku wa saa sita hatukufanikiwa kumuona basi tukafunga mlango tukalala“
Na Anna Milanzi -Katavi
Kufuatia mauaji ya Irene Yosia binti mwenye umri wa miaka 16 mkazi wa mtaa wa tulieni manispaa ya Mpanda mkoani Katavi, viongozi wa mtaa na kata ya Nsemulwa wamekemei vitendo hivyo viovu.
Mwili wa binti huyo umehifadhiwa katika makazi yake ya milele siku ya jumanne February 24, 2026 katika makaburi yaliyopo kwenye mtaa huo wa tulieni.
Mara baada ya mazishi mwenyekiti wa mtaa huo Hussein Kasomela amewataka wananchi kutoa ushirikiano ili kubaini wahamiaji katika mtaa huo.
Mtendaji wa mtaa tulieni Prosper Mwesiga amewataka wananchi wa mtaa huo kulinda amani na kujikita katika utafutaji na kila mmoja ajiandikishe katika daftari la wakazi.
Diwani wa Kata ya Nsemulwa Alex Ngereza ametoa pole kwa familia iliyofikwa na msiba huo na kusema kuwa wanaofanya vitendo hivyo hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yao
Baba mzazi ameeleza kuwa simu ya binti yake huyo ilikuwa inaita kila wakati usiku wa saa tatu na alikuwa haipokei hadi alipotoka nje ya nyumba yao na hakurejea tena ,wakamtafuta bila mafanikio hadi asubuhi alipoitwa na kuoneshwa mwili wa binti yake ukiwa katika shimo jirani na nyumba yao.