Mpanda FM
Mpanda FM
20 February 2026, 5:44 pm

“ameomba kuharakishwa kukamilika kwa ujenzi wa madarasa hayo ili kurahisisha upatikanaji wa elimu kwa wanafunzi wa eneo hilo.“
Na Ben Gadau- Katavi
Diwani wa Kata ya Ibindi Mdakuni Matongo ametembelea na kukagua ujenzi wa madarasa katika shule ya msingi muungano halmashauri ya Nsimbo iliyopo wilaya ya Mpanda mkoa wa Katavi.
Akizungumza katika eneo hilo, Mdakuni ameomba kuharakishwa kukamilika kwa ujenzi wa madarasa hayo ili kurahisisha upatikanaji wa elimu kwa wanafunzi wa eneo hilo.

Akiwa katika shule ya msingi Muungano, Mdakuni ametoa zawadi ya mipira pamoja na vifaa vingine vya michezo akisema kuwa hiyo itawasaidia wanafuzi hao kufanya mazoezi ili kujijenga na kuwa na afya bora