Mpanda FM

RC Mrindoko achukizwa, “natangaza wasimame kazi kwanza”

20 February 2026, 4:42 pm

pichani ni Mkuu wa mkoa wa Katavi (kulia) akiwa na viongozi wengine wa idara katika eneo la soko kubwa manispaa ya Mpanda

soko hilo linakabiliwa na changamoto ya uchakavu wa miundo mbinu hali ambayo inatishia usalama wa bidhaa  za wafanya biashara hususani nyakati za usiku.

Na John Benjamin -Katavi

Wafanyabiashara wa soko kubwa halmashauri ya manispaa ya Mpanda mkoani Katavi wamewaombea msamaha  wa kutosimamishwa kazi maafisa biashara,Manunuzi na Mhandisi wa manispaa hiyo kwa  kutofanya ukarabati wa soko hilo.

 Hayo yamejiri katika ziara ya mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Hoza Mrindoko alipotembelea soko hilo na kubaini kutotekelezwa kwa maagizo yake aliyoyatoa mnamo Disemba 10,2025 juu ya ukarabati wa miundombinu ya soko hilo hususani uchakavu wa paa ambayo imekuwa changamoto katika msimu huu wa masika.

Sauti ya mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko
Mkuu wa mkoa wa Katavi, Mwanamvua Hoza Mrindoko akizungumza na wafanyabiashara wa soko kubwa mkoani humo. picha na John Benjamin

Kwa upande wake mwenyekiti wa soko kubwa Bahati Issa  Ndagije  amesema soko hilo linakabiliwa na changamoto ya uchakavu wa miundo mbinu hali ambayo inatishia usalama wa bidhaa  za wafanya biashara hususani nyakati za usiku.

Nao baadhi ya wafanyabiashara wa soko hilo wamesema kuwa wamewaombea msamaha maafisa hao ili kuwapa muda wa kujitafakari na kurekebisha makosa yao tofauti na kusimamishwa kazi huenda changamoto hizo zisitatuliwe kwa wakati.

Sauti ya wafanyabiashara

Kufuatia ziara hiyo Mrindoko ametoa mwezi mmoja kuhakikisha wanatekeleza ukarabati wa miundombinu ya soko hilo.