Mpanda FM

Uelewa mdogo, umasikini vyachangia mtoto kutokupelekwa shule

12 February 2026, 1:36 pm

Anyulumye Longo Afisa Ustawi manispaa ya Mpanda, mkoani Katavi. Picha na Anna Mhina

Wazazi na walezi katika manispaa ya Mpanda, mkoani Katavi, wamesema kuwa uelewa mdogo wa jamii juu ya umuhimu wa elimu na hali ya umasikini vinachangia mtoto kutokupelekwa shule

Na Anna Mhina

Uelewa mdogo wa umuhimu wa elimu kwa watoto na hali duni ya maisha imetajwa kuwa chanzo cha baadhi ya wazazi na walezi kutowapeleka watoto wao shule.

Wakizungumza na Mpanda radio FM baadhi ya wazazi na walezi katika manispaa ya Mpanda wamesema kuwa jamii bado ina uelewa mdogo wa umuhimu wa elimu kwa watoto huku wengine wakieleza hali ya umasikini inavyochangia mtoto kutopelekwa shule.

Sauti ya wananchi na walezi

Anyulumye Longo, Afisa Ustawi manispaa ya Mpanda ameeleza umuhimu wa elimu kwa watoto mbali na kuwaongezea ujuzi na maarifa pia elimu humsaidia mtoto kutimiza ndoto zake pamoja na kumuwezesha kupata fursa mbalimbali za ajira.

Sauti ya Anyulumye Longo, Afisa Ustawi manispaa ya Mpanda

Ikumbukwe kuwa January 27, 2026 mkuu wa wilaya ya Mpanda Jamila Yusufu aliwaagiza viongozi ngazi ya mitaa na kata kupita  nyumba kwa nyumba ili kuwasaka watoto ambao hawajaripoti shule.