Mpanda FM
Mpanda FM
6 February 2026, 3:19 pm

SACP Kaster Ngonyani kamanda wa polisi Katavi. Picha na Anna Mhina
“Tumefanikiwa kuwakamata watuhumiwa 34 kwa makosa mbalimbali”
Na Anna Mhina
Jeshi la polisi mkoa wa Katavi limeendelea kuimarisha ulinzi na usalama kwa raia na mali zao kwa kufanya operasheni, doria na misako kwa lengo la kuzuia uhalifu na kufanikiwa kuwakamata watuhumiwa 34 kwa makosa mbalimbali.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake kamanda wa polisi mkoa wa Katavi SACP Kaster Ngonyani amesema kuwa kwa kipindi cha mwenzi January 2026 wamefanikiwa kuwakamata watuhumiwa 34 ambapo kati yao watuhumiwa watatu wamekamatwa wakiwa na nyara za serikali huku watuhumiwa tisa wakiwa na silaha haramu.
Katika hatua nyingine Ngonyani amesema kuwa watuhumia watatu wamekamatwa wakiwa na noti bandia kumi za dola mia moja huku wengine wawili wakiwa na ng’ombe kumi mali ya Hassan Ndege walizoiba January 27, 2026 kwa kuvunja zizi.
Hata hivyo jeshi la polisi mkoa wa Katavi limetoa wito kwa wananchi kuacha kujihusisha na vitendo viovu vya uhalifu.