Mpanda FM

Kero ya maji hospital ya Nsimbo yamkera Kimanta

22 January 2026, 5:11 pm

Kamati ya siasa ya halmashauri kuu ya Chama Cha  Mapinduzi (CCM). Picha na Samwwel Mbugi

“Tumekuja hapa tumeambiwa hakuna maji hatukubaliani na hiki kitu”

Na Samwel Mbugi

Kamati ya siasa ya halmashauri kuu ya Chama Cha  Mapinduzi (CCM) mkoa wa Katavi ikiongozwa na mwenyekiti wa chama Iddi Kimanta imeendelea na ziara ya ukaguzi wa utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi ya CCM Katika halmashauri ya Nsimbo.

Wajumbe wa kamati ya siasa wakizungumza katika ziara hiyo wameutaka uongozi wa hospitali ya halmashauri ya Nsimbo kuhakikisha wanaweka mazingira katika hali ya usafi na wezeshi kwa wagonjwa kupata huduma bila kukutana na changamoto.

Sauti ya wajumbe wa kamati

Awali akisoma tarifa kwa kamati ya siasa katibu wa afya (DHS) halmashauri ya Nsimbo Lucas Joseph Mrope amesema pamoja na kutoa huduma  za kijamii pia wanakumbana na changamoto mbalimbali ikiwemo upungufu wa watumishi kwa 75% pamoja na ukosefu wa gari la wagonjwa.

Sauti ya katibu wa afya

Hata hivyo mwenyekiti wa CCM mkoa wa Katavi Iddi Kimanta amemtaka mkuu wa mkoa kuhakikisha hospital ya halmashari inapata maji na umeme  haraka iwezekanavyo ili wagonjwa kuondokana na adha wanayokutana nayo wakati wa mahitaji muhimu.

Sauti ya Kimanta