Mpanda FM

Zijue dalili za kifafa cha mimba

15 January 2026, 3:36 pm

Dkt. Mundhiri Bashiri kutoka hospital ya manispaa ya wilaya ya Mpanda. Picha na Samwel Mbugi

“Tunaomba daktari atuelimishe kuhusu huu ugonjwa”

Na Samwel Mbugi

Kutokana na uwepo wa ugonjwa wa kifafa cha mimba katika jamii wananchi wa manispaa ya Mpanda mkoa wa Katavi wameiomba serikali kutoa elimu itakayosaidia kufahamu na kuelewa dalili na sababu zinazosababisha.

Wameyasema hayo wakizungumza na Mpanda Radio FM ambapo wameiomba serikali kutoa elimu itakayosaidia kufahamu ugonjwa huo inasababishwa na nini pamoja na viashiria vya kupata kifafa cha mimba.

Sauti za wananchi

Kwa upande wake Dr. Mundhiri Bashiri kutoka hospital ya manispaa ya wilaya ya Mpanda amesema ugonjwa huo anaweza kumpata mama mjamzito na dalili za kifafa cha mimba ni mgonjwa kuonyesha dalili za degedege.

Sauti ya daktari

Hata hivyo Dr. Mundhiri amesema ugonjwa huo huwa unasababishwa na kondo la nyuma la mtoto likipata shida wakati wa kujitengeneza.

Sauti ya daktari

Ugonjwa wa kifafa cha mimba ni miongoni mwa magonjwa hatari sana kwa maisha ya wanawake wengi wajawazito nchini Tanzania.